



Wednesday 02-
BIHARAMULO
Halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani kagera inatarajia kuitumia zaidi ya shilingi milioni 290 kwa ajili ya kutengeneza barabara za wilaya hiyo zenye urefu wa kilomita 120
Mhandisi wa ujenzi wa halmashauri ya wilaya ya Biharamulo Bw Mahona Sambo amesema shilingi milioni 53 kati ya hizo zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara za mjini
Amesema fedha zilizobaki zitafanya matengenezo ya barabara na makalvati katika maeneo ya vijijini
Bw sambo amesema kazi hizo ambazo zitafanyika mwaka huu zitatahusu matengenezo ya kawaida, maeneo korofi pamoja na ujenzi wa Makalvati
NGARA
Mganga wa hospitali ya Nyamiyaga wilayani Ngara, Bw. Misago Senyamanza, ametangaza nia ya kugombea nafasi ya udiwani wa kata ya Mugoma, wilayani humo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Bw. Misago, ambaye ametangaza kugombea kupitia chama cha mapinduzi CCM amesema ameamua kuwania nafasi hiyo ili kushirikiana na wakazi wa kata ya Mugoma kuharakisha maendeleo yao.
Amesema maendeleo ya kata hiyo yamebaki nyuma kwa muda mrefu hivyo ameahidi kuwa endapo atachaguliwa atashirikiana na wakazi wa kata hiyo kuharakisha maendeleo
Bw. Misago, aanakuwa mwana CCM wa pili kutangaza nia ya kugombea udiwnai wa kata ya Mugoma baada ya Diwani wa sasa Bw George Rubagora kutangaza pia nia ya kutaka kuendelea na wadhifa huo.
KASULU
Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa mataifa UNICEF linatarajia kuanza kutoa mafunzo ya stadi za maisha kwa watoto wanaoishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Mtabila iliyoko wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Mkuu wa makazi wilayani Kasulu Bw Fredrick Nsajile amesema hayo katika kikao cha kutambulisha mpango huo wa UNCEF ulioanzishwa baada ya kubaini kuwa watoto wa kambi hiyo wanaishi katika mazingira hatarishi
Amesema kambi hiyo iliyofungwa rasmi june 30 mwaka jana haina shule hivyo watoto kukosa cha kufanya na wengine kwenda kufanya kazi katika maeneo mbalimbali
Bw Nsajile amesema UNICEF imechukua jukumu hilo ili kuwasaidia watoto wanaojiingiza katika vitendo viovu kama vile kuvuta bangi na wizi kutokana na kukosekana kwa mfumo rasmi wa elimu
Kambi ya mtabila iliyofungwa mwaka jana ina jumla ya wakimbizi elfu 36 na kati yao watoto ni aslimia 50
NGARA.
Mkazi wa Kijiji cha Kanazi Wilayani Ngara Gilbert Nyamblomba amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitano gerezani baada ya kupatikanana hatia ya kujaribu kuiba Pikipiki
Akisoma hukumu hiyo hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Ngara, Bw Geofrey Biyereza amesema mahakama imetoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka.
Awali mwendesha Mashitaka wa polisi Bw. John Kessy amesema mshitakiwa alitenda kosa hilo March 11 katika kijiji cha Kanazi wilayani Ngara
Amesema mshitakiwa alitaka kunyang’anya pikipiki aina ya Sanlag yenye namba za usajili T. 495 BCM mali ya Bw. Oswad Nyamlomba ambaye ni ndugu yake
MULEBA
Wanachama wawili wa CCM, Prof Anna Tibaijuka na bw Alfred Tibaigana wametangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Muleba Kusini linaloongozwa na Bw Wilson Masilingi.
Bw Tibaigana ambaye alikuwa Kamanda Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amekabidhi
barua yake kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Wilbroad Musafiri, muda mfupi baada
ya Prof Tibaijuka kutangaza nia
Bw Tibaigana amekanusha uvumi ulioeneka kw awananchi kwmaba amejiondoa katika kinyang’anyiro hicho
Amesema kuna kundi linalosambaza uvumi kuwa amebadili nia, huku akidai kuwa baadhi yao wanawapotosha wananchi kuwa atakwenda kugombea jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam.
ARUSHA
Waziri Mkuu, Bw Mizengo Pinda, amesema ni muhimu kwa wananchi wa Afrika Mashariki kuelezwa maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili waweze kunufaika nayo.
Bw Pinda amesema hayo jana wakati alipotembelea kuona ujenzi wa makao makuu ya ofisi za Jumuiya hiyo unaondelea mjini Arusha.
Amesema wananchi ambao ndio wenye Jumuiya waelezwe kila hatua na wafahamu mwelekeo wa jumuiya ili waweze kunufaika
Aidha waziri mkuu amesema kuanza kwa ujenzi huo kunaonyesha dhamira ya viongozi wa nchi tano wa Jumuiya hiyo kwa kujenga umoja kati yao wenye nguvu na kuwaletea maendeleo wananchi wao.
KIGALI
Wakili wa Mwanasiasa wa Rwanda Bi Viktwar Ingabire amepelekwa hospitali baada ya kulalamika kuwa na matatizo ya moyo
Wakili huyo Peter Elinder ambaye anashikiliwa kwa tuhuma za kukanusha kuwepo kwa mauaji ya halaiki, alipelekwa katika hospitali ya Mfalme Faisal mjini Kigali ambako uchunguzi ulionyesha kwamba hana tatizo la moyo kama alivyodai
Maofisa wa polisi wa Rwanda wamesema, Wakili huyo raia wa marekani anaendelea kuhojiwa kabla ya kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kukanusha kuwepo kwa mauaji ya halaiki ya mwaka 1994
Bw Elinder aliingia nchini Rwanda wiki moja iliyopita ili kumwakilisha Bi Ingabire
ambaye pia anakabiliwa na mashitaka ya kukanusha kuwepo kwa mauaji ya halaiki pamoja
na kushirikiana na makundi ya magaidi
29th May 2010
BIHARAMULO
Mkazi wa kata ya Runazi wilayani Biharamulo mkoani kagera amaefikishwa katika mahakama ya wilaya hiyo akikabiliwa na tuhuma ya kumtorosha mwanafunzi wa darasa la tano wa shule ya msingi Mlimani
Mbele ya hakimu Gabriel Mariki Mwendesha mashitaka wa polisi bwa Boniface Mayala amemtaja mshitakiwa kuwa ni Hamis Ramadhani
Amesema mshitakiwa alitenda kosa hilo May 15 mwaka huu katika eneo la Kijiji cha Ng’ambo wilayani Biharamulo ambako alimchukua msichaan huyo na kumepeleka katika kata ya Runazi
Amesema mshitakiwa alimtorisha msichana huyo kwa lengo la kufanyia kazi za ndani
Mshitakiwa amekana shitaka lake na kupelekwa rumande ambapo kesi yake itatajwa tena June tisa mwaka huu.
...........................................................................................
NGARA
Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Ngara wameipongeza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa uamuzi wake wa kuwahoji wanasiasa wanatoa pikipiki, baiskeli na zawadi nyingine katika majimbo.
wakazi hao wamesema hayo kufuatia maelezo yaliyotolewa jana Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru,
Dk Edward Hoseah kuwa taasisi yake ina orodha ya waliogawa pikipiki, baiskeli na
zawadi nyingine
Wakiongea na radio kwizera kwa nyakati tofauti wakazi hao wamesema baadhi ya watu waliotangaza nia ya kugombea ubunge wilayani humo wamekuwa wakitoa vitu mbalimbali kinyume cha sheria
Wakazi hao wamesema hatua hiyo ya TAKUKURU inapaswa kuchukuliwa haraka ili kudhibiti vitendo hivyo na kuwa zawadi hizo hutolewa kwa nia mbaya kwani hulenga makundi fulani ya watu
.................................................................................................................................................
BIHARAMULO
Watoto watatu wa familia moja katika kijiji cha Katerela, Kata ya Biharamulo
mjini mkoani Kagera wameteketea kwa moto walipokuwa wamelala usiku wa kuamkia juzi
Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Bw Henry Salewi, amesema tukio hilo limetokea wakati
watoto hao wakiwa wamelala kwenye nyumba peke yao, kwani wazazi wao walikuwa wamelala
nyumba ya jirani.
Kamanda Salewi amesema, jitihada za kuwaokoa watoto hao zilishindikana kutokana na
moto kuwaka kwa kasi katika nyumba hiyo
Pia amesema uchunguzi wa awali wa tukio hilo unaonyesha watoto hao walilala usingizi
na kuacha moto walioukoka wenyewe ukiendelea kuwaka kwenye jiko la mafiga na baadaye
kushika kwenye nyasi za nyumba hiyo.
.................................................................................................................................................
MISUNGWI
Mamia ya watu wakiwa na silaha za jadi wamevamia na kuvunja kituo cha kidogo cha polisi cha kata ya Mbarika, wilayani Misungwi mkoani mwanza na kuwaua watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi.
Tukio hilo limetokea juzi saa 1:30 jioni wakati raia hao wakiwa na silaha kama vile mapanga, rungu na mawe walipovamia kituo hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Siro, askari polisi wawili wa kituo hicho, walizidiwa nguvu na wananchi hao, hali iliyosababisha kukimbia ili kuokoa maisha yao.
Amesema Majambazi hayo yalikamatwa wakati yakijiandaa kufanya uhalifu na kufikishwa kituoni hapo lakini baadaye wananchi walivamia kituoni na kuwaua watu hao
.................................................................................................................................................
DAR ES SALAAM
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imelikataa ombi la viongozi wa dini kutaka uchaguzi mkuu ujao usifanyike siku ya Jumapili kama ilivyopangwa na tume hiyo.
Mkurungezi wa Uchaguzi, Bw Rajabu Kiravu, iamesema uamuzi huo umezingatia utamaduni wa muda mrefu wa kupiga kura siku ya Jumapili.
Amesema tangu Tanzania ipate Uhuru mwaka 1961, chaguzi zote zimekuwa zikifanyika siku ya Jumapili, isipokuwa mwaka 2005 ambapo tume hiyo, ililazimika kuahilisha kutokana na kifo cha mmoja wa wagombea
Amesema kwa kawaida vituo vya kupiga kura hufunguliwa kuanzia saa 1.00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni na kuwa mpiga kura anaweza kuweka utaratibu wa muda ambao ataona unamwezesha kusali na kupiga kura
.................................................................................................................................................
KINSHASA
Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limepiga kura ya kuidhinisha kuondolewa kwa walinzi wake elfu mbili kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo DRC ifikapo June 30 mwaka huu
Hata hivyo baraza hilo limeahirisha uamuzi wa kuwaondoa askari wake elfu 20,500 kama ilivyopendekezwa na Rais Joseph kabila wa DRC
Uamuzi wa kuwaondoa asakari wote wa umoja wa mataifa kutoka DRC utatolewa mwaka ujao kwa kuzingatia hali ya usalama ilivyo nchini humo
Kadhalika baraza hilo limeongeza muda wa vikosi vya ke nchini DRC hadi June 30 mwaka kesho
.................................................................................................................................................
KIGALI
Jeshi la Polisi nchini Rwanda Jana limemkamata wakili Peter Erlinder kutoka marekani kwa tuhuma za kukanusha kuwepo kwa mauaji ya halaiki
Wakili huyo amewasili nchini humo kwa ajili ya kumtetea mwanasiasa Bi Viktwar Ingabire anayeshitakiwa kwa ugaidi na kukanusha kuwepo kwa mauaji ya halaiki ya mwaka 1994 ambapo zaidi ya wtau laki tano waliuawa
Msemaji wa Jeshi la Polisi la Rwnada Bw Eric Kayiranga amesema wakili huyo amekamatwa jana asubuhi
Amesema wakili huyo kutoka Marekani anatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya kukamilika kwa uchunguzi
...................................................................................................................................................................................
NEW YORK
Wanachama wa mkataba wa kuzuia usambazaji wa silaha za nyuklia wamekubaliana kuhakikisha kuwa eneo la mashariki ya kati halina silaha za nyuklia
Wanachama wa mkataba huo waliokutana mjini New York wametaka kuitishwa mkutano mwaka 2012 ambapo nchi za mashariki ya kati ikiwa ni pamoja Iran zitakutana kufikia azma hiyo
Aidha makubaliano hayo yameitaka Israel kujiunga katika mkataba wa kuzuia kusambaa kwa silaha za nyuklia
Rais Barack Obama wa Marekani ameunga mkono hatua hiyo lakini amepinga hatua ya kutengezwa kwa Israel kwani italipelekea taifa hilo kushbindwa kuhudhguria mazungumzo ya mwaka 2012
Kikwete Na Ardhi.
Rais Jakaya Kikwete, amewaagiza wananchi wanaoishi kandokando ya barabara za lami nchini kutokubali kurubunika kuuza mashamba yao kwa wageni kwa lengo la kuwekeza.
Rais Kikwete ametoa agizo hilo jana wakati wa uzinduzi wa barabara ya Horohoro Tanga yenye urefu wa kilomita 65 itakayojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi bilioni 78.05.
,Rais Kikwete amesema kutokana na kuboreka kwa barabara nchini watu kutoka maeneo mbalimbali watafika katika eneo la kijiji cha Mikocheni wilaya ya Tanga kwa nia ya kutaka kuwekeza.
Amesema wananchi wanapaswa kuchangamkia fursa za kiuchumi za nchi za Afrika Mashariki zitakazotokana na kuimarika kwa barabara zilizo karibu na maeneo yao ili waweze kujikwamua na umaskini .
Rais Kikwete ameishukuru Serikali ya Marekani kwa kutoa kiasi cha dola milioni 698 kupitia taasisi ya Millenium (MCC) kwa kipindi cha miaka mitano katika shughuli za maendeleo nchini.
Barabara hiyo inajengwa na Kampuni ya Sinohydro Corparation Ltd kutoka nchini China ambayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika Aprili 2012.EndS
.......................................................................
KIBONDO
Uongozi wa zahanati ya Rugunga kata ya Kitahana wilayani Kibondo umeiomba halmashauri ya wilaya hiyo kujenga choo na tanuru la kuchomea taka.
Mganga mfawidhi wa zahanati hiyo Bw William Kanyungu amesema choo cha zahanati hiyo kilichojengwa mwaka 1983 kinakaribia kujaa
Naye mhudumu wa afya katika zahanati hiyo Bi Liberatha Nchana amesema wanahitaji tanuru la kuchoma takataka zinazopatikana katika zahanati yao
Aidha Bi Nchana amesema takataka zote zinatakiwa zichomwe moto hivyo halmashauri haina budi kushughulikia tatizo hilo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza
NGARA.
Mkazi wa Kijiji cha Kanazi Wilayani Ngara Gilbert Nyamblomba amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitano gerezani baada ya kupatikanana hatia ya kujaribu kuiba Pikipiki
Akisoma hukumu hiyo hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Ngara, Bw Geofrey Biyereza amesema mahakama imetoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka.
Awali mwendesha Mashitaka wa polisi Bw. John Kessy amesema mshitakiwa alitenda kosa hilo March 11 katika kijiji cha Kanazi wilayani Ngara
Amesema mshitakiwa alitaka kunyang’anya pikipiki aina ya Sanlag yenye namba za usajili T. 495 BCM mali ya Bw. Oswad Nyamlomba ambaye ni ndugu yake
KIBONDO
Serikali wilayani Kibondo imewataka wakazi wa wilaya hiyo kupanda miti na kuacha tabia ya kilimo cha kuhama hama ili kudhibiti uharibifu wa mazingira
Mkuu wa wilaya ya Kibondo Bw Dan Makanga amesema hayo jana wakati akizindua maadhimisho ya siku ya mazingira duniani ambayo wilayani Kibondo imefanyika katika kijiji cha Biturana
Katika hotuba iliyosmwa kwa niaba yake na Katibu tawala wa wilaya ya Kibondo Bw Julius Samwely, mkuu huyo wa wilaya amesema jamii iepuke tabia za kukata miti ovyo, kuchoma moto na kulima katika vyanzo vya maji
Kauli mbiu ya mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya mazingira ni “Tunza mazingira ya asili kwa hifadhi endelevu ya viumbe hai” EndS
MULEBA
Wanachama wawili wa CCM, Prof Anna Tibaijuka na bw Alfred Tibaigana wametangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Muleba Kusini linaloongozwa na Bw Wilson Masilingi.
Bw Tibaigana ambaye alikuwa Kamanda Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, amekabidhi
barua yake kwa Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Wilbroad Musafiri, muda mfupi baada
ya Prof Tibaijuka kutangaza nia
Bw Tibaigana amekanusha uvumi ulioeneka kw awananchi kwmaba amejiondoa katika kinyang’anyiro hicho
Amesema kuna kundi linalosambaza uvumi kuwa amebadili nia, huku akidai kuwa baadhi yao wanawapotosha wananchi kuwa atakwenda kugombea jimbo la Kawe jijini Dar es Salaam.
BUNDA.
Mkazi wa Kibara wilayani Bunda mkoani Mara amejinyonga hadi kufa kwa kutumia kamba kutokana na kinachosadikiwa kuw ani ugomvi wa kimapenzi
Kamanda wa polisi mkoani Mara Bw Robert Boazi amesema tukio hilo limetokea May 31 katika wilaya ya Musoma vijijini ambako mtu huyo alikwenda kwao na mke wake aliyetambuliwa kuwa ni Esther Daniel.
Kamanda Boazi amemtaja aliyejinyonga kuwa ni Paul Ngawia mwenye umri wa miaka 30 ambaye kabla ya atukio hilo alikuwa ametengana na mke wake na alikuwa amekwenda kumtaka mkewe arejee nyumbani.
Amesema hakuna mtu aliyekematwa kuhusu tukio hilo na kwmaba polisi wanaendelea kufanya uchunguzi
DODOMA
Kanisa la Anglikana Tanzania (ACT) limesema litawanyang’anya mavazi ya kiaskofu ambayo
yamekuwa yakitumiwa vibaya na watu wanaojiita maaskofu wa Kanisa jipya la Kiinjili
la Anglikana Tanzania.
Katibu Mkuu wa kanisa hilo, Dk. Mwita Akiri, ametoa taarifa hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu habari kuwa kanisa hilo limemeguka
Dr Akiri amesema wataandika barua kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Msajili
wa Vyama vya Hiari ili wasisajili kanisa hilo mpaka litakapofuta jina la Anglikana,
kwani liko kinyume cha taratibu za usajili.
Amesema Serikali itasaidia kuwapa uelewa
wananchi kuhusu ujio wa Kanisa hilo lenye lengo la kuleta uvunjifu wa amani kwa Kanisa
Anglikana Ends
KIGALI
Zaidi ya raia elfu 17 wa Rwanda wanaoishi nje ya nchi hiyo wamejiandikisha kwa ajili ya kupiga kura kwenye uchaguzi wa rais wa taifa hilo uliopangwa kufanyika mwezi Augist mwaka huu
Katibu mtendaji wa Tume ya uchaguzi ya Rwanda Bw Charles Munyaneza amesema jana kuwa idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka
Amesema idadi hiiyo imeongezeka kutoka elfu 16 waliojiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi wa rais wa Mwaka 2003
Bw Munyaneza amesema tume ya uchaguzi ya Rwanda itaendelea kuwahamaisha raia wake walioko ndani na nje ya nchi ili kushiriki uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Agiost tisa mwaka huu